Burudani

Maisha ya ‘usela’ yamtoa machozi Snura

Mvumilivu hula mbivu. Snura amefunguka kuwa shida alizozipitia ndio sababu kubwa kwake kuweza kufika alipokuwa sasa kimafanikio ya maisha.

Muimbaji huyo amesema wakati alipoamua kutoka nyumbani kwa wazazi na kwenda kuanza maisha yake mwenyewe alifikia kipindi alikuwa anashinda na njaa na wakati mwingine alishindia ugali na mbilimbi.

Akiongea na Magic FM, hitmaker huyo wa Shindu amesema, “Nilishalala njaa sana tu, tena sana wakati natoka kwa wazazi na kuanza maisha yangu binafsi ya kujitegemea. Nilikuwa na wakati mgumu sana nakumbuka nilikuwa nashindia ugali na mbilimbi na nilikuwa jeuri kwa sababu maisha hayo hayakufanya nimtegeme mwanaume.”

“Nilikuwa jeuri kwa sababu maisha hayo hayakufanya nimtegeme mwanaume. Mimi nilikuwa jeuri sana japo nilikuwa na shida zangu. Ila kati ya vyote suala la kodi nilikuwa linaniumiza kichwa vibaya sana, mawazo yalikuwa yanaongezeka mara mia kila nikifikiria kodi ya baba mwenye nyumba na kipindi hicho nakumbuka kodi ilikuwa 20,000 kwa mwezi ila ilikuwa mbinde kuipata,” ameongeza.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents