MAMAs 2009 ndani ya Nairobi
MTV Afrika wametangaza kuwa tuzo za MTV Africa Music Awards 2009
zitafanyika jijini Nairobi tarehe 10 Oktoba ndani ya ‘Moi International
Sports Centre’, na wanatarajia itawafikia watu bilioni 1 kwa kupitia
runinga (TV)
Kampuni ya Zain amabayo ni mdhamini wa tuzo hizo imetangaza kwamba siku hiyo wataandika historia
Mwaka jana Bongo iliwakilishwa na Professor Jay katika tuzo hizo ambazo zilifanyika nchini Nigeria..je mwaka huu nani atatuwakilisha?
Wakali wengine waliyokwepo mwaka jana ni Kelly Rowland, Flo Rida, The Game, Jua Cali, P Square, 9ice, D’Banj, Asa, Cassette na Jozi.
MTV Africa Music Awards zitaoneshwa Afrika nzima tarehe 17 Oktoba 2009 kwa kupitia DStv (Channel 322), Daarsat, WBS (Uganda), TBC (Tanzania), TV3 (Ghana), STV (Nigeria) na AIT (Nigeria).