Michezo
Man United, Madrid, Juventus na timu nyingine 4 zaungana na Barcelona hatua ya 16 bora UEFA
Jana usiku klabu 7 zimefuzu kwenye hatua ya 16 bora ya klabu bingwa barani Ulaya na kuungana na klabu ya Barcelona ambayo ndio ilikuwa timu ya kwanza kufuzu kwenye michuano hiyo.
Klabu hizo ni Real Madrid, Ajax, Bayern Munich, Manchester United, AS Roma, Juventus na Manchester City.
Real Madrid, Manchester United, Juventus, Ajax na Bayern Munich zimefuzu kwa matokeo ya ushindi usiku wa jana.