Dhamana ya Mhe. Mbowe na Esther Matiko yampeleka Zitto Kabwe mahakamani
Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amesema kuwa leo Novemba 28, 2018 atafika katika Mahakama Kuu kuonesha mshikamano, kufuatia kunyimwa dhamana kwa Kiongozi wa CHADEMA, Freeman Mbowe na Mbunge Esther Matiko.
Zitto amesema anaenda kuungana na viongozi kuonyesha mshikamano dhidi ya vitendo vya kibabe, kikatili na ukandamizaji wa haki.
Viongozi na Wabunge wenzangu @freemanmbowetz na @esthermatiko watakuwa mahakama Kuu leo asbh hii kwa rufaa yao dhidi ya kufutiwa dhamana. Nitakuwepo kuonyesha mshikamano dhidi ya vitendo vya kibabe, kikatili na ukandamizaji wa haki.
— Zitto MwamiRuyagwa Kabwe (@zittokabwe) November 28, 2018
Wiki iliyopita, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ilimfutia dhamana mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema, Freeman Mbowe na Ester Matiko kwa kukiuka masharti ya dhamana yao.