Habari

Marekani yasitisha mashirika ya ndege China, mvutano waendelea

Mvutano kati ya mataifa makubwa yanayoshikilia uchumi wa Dunia, China  na  Marekani unaendelea  kuwapo, ambapo hapo  jana Jumatano utawala wa Rais Trump umeamuru  kusitishwa kwa  safari  zote  za  ndege  za  mashirika  ya  ndege  ya  China kwenda  na  kutoka  Marekani.

Trump administration denies Chinese airlines entry into U.S. ...

Wakati hayo yakijiri upande wa China  hii leo imesema kuwa itaruhusu ndege  za  kigeni ambazo  zimezuiwa  hivi  sasa kufanyakazi  nchini  humo  kuanza  safari za  abiria  kuanzia  Juni 8, na  kuondoa marufuku kwa  ndege  za  Marekani.

Waandamanaji mjini Hong Kong

Wakati  huo huo  bunge  la  Hong Kong limepitisha  sheria tata ya mswada wa  wimbo wa taifa leo ambao utafanya  kutoheshimu wimbo wa  taifa  wa  China  kuwa  ni  kosa  la  jinai, hatua  ambayo wakosoaji wanaiona kuwa  ishara  ya  hivi  karibuni  kabisa  ya Beijing  kukaza kamba katika  mji  huo. Uamuzi  huo  unaweza kuzusha  maandamano zaidi katika  mji  huo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents