Michezo
Mashabiki wa Man United waelekeza hasira zao kwa David Moyes na Sir Alex Ferguson baada ya kufungwa na Man City 3-0
Kichapo cha bao 3-0 walichopata jana kutoka kwa Manchester City kimewakasirisha mashabiki wa Manchester United, na wameamua kuelekeza hasira zao kwa kocha Davidi Moyes na Sir Alex Ferguson.
Shabiki akimtukana David Moyes
Kufungwa huko kulipandisha hasira za mashabiki wa timu hiyo ambapo wale waliokuwa karibu na David Moyes walilazimika kushikwa na walinzi wakitaka kumshambulia huku wengine wakielekeza hasira zao kwa Ferguson.
Shabiki huyu aliamua kuinuka kwenye kiti chake kumtukana Moyes na hivyo kuondolewa na walinzi
David Moyes akiwa na huzuni baada ya kichapo cha bao 3-0
Mashabiki wanalaumu uamuzi wa Ferguson kumwachia mikoba Moyes kama kocha wa Manchester United.