Matokeo ya mechi za UEFA Feb 17 Roma vs Real Madrid,Gent na Wolfsburg
Michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ilichezwa usiku wa February 17 mechi kati ya Gent dhidi ya Wolfsburg na mchezo kati ya Real Madrid dhidi ya AS Roma ya Italia, ilikamilisha idadi ya timu 8 za kwanza kucheza mechi zake za kwanza za hatua ya 16 bora.
Cristiano Ronaldo akishangilia goli pamoja na kocha wake
Mchezo uliokuwa unasubiriwa kwa hamu usiku wa February 17 wa Ligi ya Mabingwa Ulaya ni mchezo kati ya Roma dhidi ya Real Madrid.
Mchezo wa Real Madrid ya Hispania ulimalizika kwa ushindi wa goli 2-0, licha ya AS Roma kuwa katika uwanja wao wa nyumbani, Goli la kwanza la Real Madrid lilifungwa dakika ya 57 na Cristiano Ronaldo na Jesse Rodriguez alifunga goli la pili dakika ya 86.
Mchezaji Julian Draxler wa Wolfsburg akishangilia goli
Namchezo kati ya Gent na Wolfsburg ulimalizika kwa Gent 2 – 3 Wolfsburg.