Habari

Mauritius kusaidia ulinzi teknolojia Tz

tehnohama

 

SERIKALI ya Mauritius  imeonyesha nia ya kuisaidia Tanzania  katika kuimarisha ulinzi wa Teknolojia ya habari na Mawasiliano (Teknohama) ambapo  pamoja na mambo mengine, utaalamu huo utaliwezesha Taifa kupiga hatua kubwa  katika upande huo.

Hayo yamesemwa jana na Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia Makame Mbarawa, mara baada ya ziara yake katika Taasisi ya teknolojia ya Dar es salaam (DIT) akiambatana  na Waziri wa Elimu, Sayansi na utafiti wa teknolojia wa Mauritius Dkt. Rajesh Jeetah.

Mbarawa alisema wakati huu ambapo Tanzania inazidi kujiimarisha katika nyanja ya teknolojia, Serikali ya Mauritius tayari ilishafanikiwa  katika suala hilo  hivyo ushirikiano wa kimawasiliano ambao Mataifa yote mawili yameuonyesha, utalisaidia Taifa letu kufikia  kiwango kizuri.

Aidha amewataka wataalamu wa masuala mbalimbali kutojificha badala yake wajitokeze kwa wananchi ili waweze kuwasaidia katika masuala waliyobobea ambapo kwa kufanya hivyo alisema kutasidia kuondoa mapungufu wa wataalamu, kama hali ilivyo sasa.

Kwa upande wake Waziri wa Elimu, Sayansi na utafiti wa teknolojia wa Mauritius Dkt. Rajesh Jeetah, alisema nchi yake kwa sasa imejidhatiti katika masuala mbalimbali ya teknolojia zikiwemo za mawasiliano na uendeshaji wa mitambo, hivyo inataka ibadilishane utalaamu ilionao na Tanzania.

Alisema kwa kuanza Serikali yake imechukua jukumu la kuwafundisha watalaam saba ambao mara baada ya mafunzo hayo watakayoyapewa  wataweza kushirikiana na wataalamu wengine waliopo nchini katika nyanja nzima ya teknohama.

 

 

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents