Michezo

Mbappe afunguka na kuwabeza Messi, Ronaldo, Neyamar na Buffon amtaja mchezaji bora wa muda wote

Mbappe afunguka na kuwabeza Messi, Ronaldo, Neyamar na Buffon amtaja mchezaji bora wa muda wote

Mchezaji wa klabu ya PSG na taifa la Ufaransa Kylian Mbappé Lottin amefunguka na kuwabeza wachezaji ambao wanasemekana ni bora kwa sasa duniani.

Mbappe ameongea hayo akifanya mahojiano na ESPN na kuwabeza akina Lionel Messi,Cristiano Ronaldo na Neymar ambaye anacheza nae kalbu moja ya PSG na kusema hakuna mchezaji bora kama Pele duniani.

Mbappe aliongeza ili kumpata mchezaji bora kama Pelle ni lazima uwachanganye wachezaji wanne wa sasa kwa kufanya haya.

“Messi ntachukua mguu wa kushoto, Neymar ntachukua mguu wa kulia Ronaldo ntachukua uwezo wake wa kufikiri na Buffon ntachukua busara zake nido unamtengeneza mchezaji mmoja mwenye uwezo wa Pelle”

Na baada ya kuulizwa nafasi ya Mbappe iko sehemu gani hapo alisema ” Haina haja hiyo imekamilika kabisa imekaa vizuri”

“Kiukweli nina furaha sana najivunia kwake lakini huu ni mliganisho mgumu na mzuri unaofaa kabisa”

“Sidhani kama kuna mchezaji atafanya kama Pelle alivyofanya kipindi hicho,Kuna Pelle mmoja tu duniani alikuwa wa kitofauti’

Mbappe aliongeza “Siumizi sana kichwa kuhusiana na hili kumtambua nani bora,kwa sababu hakuna mchezaji atakayeweza kumfikia Pelle”

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents