Burudani

Mbosso aanza kuchekelea mafanikio WCB 

Usiku wa kuamkia January 29 mwaka huu label ya WCB walimtambulisha msanii mpya ambaye ni Mbosso aliyekuwa Yamoto Band.

Licha ya Mbosso kutambulishwa usiku huu pia siku hii hiyo ndipo wimbo wake wa kwanza ‘Watakubali’ ulitoka official baada ya hapo awali kushirikishwa na WCB katika ngoma yao ya pamoja ‘Zilipendwa’.

Ikiwa ni zaidi ya wiki moja tangu wimbo huo utoke, leo February 8 umeweza kufikisha views milioni moja katika mtandao wa YouTube kitu ambacho Mbosso anasema hakuwahi kukifikiria.

“Sikuwahi kufikiria hata siku moja kama na Mimi kuna siku nitatoa wimbo wangu na ukapokelewa kwa mikono miwili kiasi hichi, ni Baraka tu za Mwenyezi Mungu na support kubwa mnayonipa wadau na mashabiki wa mziki,” amesema .

Video ya Mbosso ‘Watakubali’ ilitoka January 28 mwaka huu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents