Michezo

Mchezaji ‘The Juice’ aachiwa huru kifungo cha miaka 33

O.J. Simpson maarufu kama The Juice ambaye ni mchezaji wa zamani wa soka la Marekani na muigizaji, amesamehewa kifungo chake cha miaka 33 alichohukumiwa.

Jopo linalohusika na msamaha kwa wafungwa limefikia maamuzi hayo kwa The Juice mwenye umri wa miaka 70 ambaye alihukumiwa kifungo hicho katika gereza la Nevada na tayari alishakuwa ametumikia kifungo cha takribani miaka tisa.

Mchezaji huyo alikuwa akishtakiwa kwa makosa yapatayo 10 ambapo kubwa zaidi likiwa la uvamizi wa hoteli ya Las Vegas mwaka 2007. Wakati huo huo mwaka 1995 mzee huyo aliwahi kushtakiwa kwa kosa la mauaji ya aliyekuwa mkewe, Nicole Brown Simpson na rafiki yake Ron Goldman hata hivyo aliachiliwa.

Kwa sasa The Juice ataachiwa huru rasmi ifikapo mwezi Octoba ya mwaka huu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents