Michezo

Mchezaji wa Arsenal Kolasinac aandika ujumbe huu baada ya kuvamiwa na vibaka barabarani akiwa na Ozil (+ Video)

Mchezaji wa Arsenal Kolasinac aandika ujumbe huu baada ya kuvamiwa na vibaka barabarani akiwa na Ozil (+ Video)

Wachezaji nyota wa Arsenal Mesut Ozil na Sead Kolasinac wameripotiwa kuvamiwa na genge la majambazi katika jaribio la wizi wa gari katika barabara za mji wa London.

Klabu ya Arsenal imethibitisha kuwa wachezaji wake Mesut Ozil na Sead Kolasinac walilengwa na majambazi hao waliokua wamejihami lakini hawakujeruhiwa katika tukio hilo.

Ozil and KolasinacHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionSead Kolasinac na Mesut Ozil

Kanda ya video iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii inamuonesha Kolasinac akipigana na na wanaume wawili waliokuwa wamejihami kwa visu.

Mchezaji huyo pia anaonekana akiruka kutoka kutoka kwenye gari kukabiliana na wanaume waliokuwa wameficha nyuso zao na ambao walikuwa na njama ya kuwaibia.

Msemaji wa polisi wa jiji la London amesema: “Tumepata taarifa kuwa washukiwa waliokuwa juu ya pikipiki walijaribu kumuibua mtu aliyekuwa akiendesha gari.

“Dereva pamoja na abiria wake walifanikiwa kuondoka eneo la tukio bila kujeruhiwa na kwenda hadi eneo la Golders Green, ambako wamewasilisha taarifa kwa maafisa wetu.”

Hakuna mshukiwa yeyote aliyekamatwa kufikia sasa .

Kolasinac na Ozil ni wachezaji wa kwanza wa soka kuvamiwa katika barabra za London.

Mwaka 2016, aliyekuwa wakati huo mshambuliaji wathen West Ham Andy Carroll alitishiwa kwa bunduki alipokuwa njiani kwenda nyumbani kutoka mazoezini.

Baada ya tukio hilo Kolasinac ameandika ujumbe huu kwenye ukurasa wake wa Twitter,

https://twitter.com/seadk6/status/1154708968033411073

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents