Mchezaji wa Tottenham Hotspurs atalii mbuga za wanyama nchini
Siku chache baada ya mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Uingereza na klabu ya Manchester united, David Beckham kutua nchini Tanzania kwa ajili ya kutalii akiwa na familia yake. Na kuwasili nchini kwa Mfaransa, Mamadou Sakho beki wa Liverpool kwa ajili ya kutalii mkoani Arusha na kutazama namna Tanzania ilivyobarikiwa na maliasili.
Mchezaji wa Tottenham Hotspurs ya Uingereza na timu ya Taifa ya Denmark Christian Eriksen.
Ujio wa wachezaji hawa ni kama kumezidi kuifungulia milango Tanzania katika sekta ya utalii baada ya safari hii kupata ujio wa Mchezaji wa klabu ya Tottenham Hotspurs ya Uingereza na kiungo wa timu ya Taifa ya Denmark Christian Eriksen.
Mchezaji wa Tottenham Hotspurs ya Uingereza na timu ya Taifa ya Denmark Christian Eriksen
Mbali ya Christian Eriksen, mchezaji raia wa Kenya na klabu ya Spurs Victor Wanyama naye amewasili nchini kwaajili mapumziko yake.
Mchezaji raia wa Kenya na klabu ya Spurs Victor Wanyama akitua nchini
Christian Eriksen amekuwa tofauti kidogo na mchezaji Mamadou Seakho ambaye alikuwa haoni tabu kuposti picha zake na kuandika kuwa yupo Tanzania
BY HAMZA FUMO