Burudani
Mez B kuzikwa leo mjini Dodoma
Maelfu ya wakazi wa mjini Dodoma leo wameshiriki kumuaga msanii wa R&B, Moses Bushagama aliyejulikana zaidi kwa jina la Mez B.
Mwili wake ulianzwa kuagwa kuanzia midaa ya saa sita mchana kwenye viwanja vya Nyerere Square mjini humo.
Ibada ya mazishi inafanyika kwenye makaburi ya wahanga, Maili Mbili mjini humo ambako ndiko atakapozikwa.
Wasanii mbalimbali wamehudhuria mazishi yake.