Mikoa 9 kukumbwa na Mvua kubwa nchini, TMA yatoa tahadhari na athari zitakazo jitokeza
Mamlaka ya hali ya hewa nchini (TMA), imetoa utabiri wa siku tano leo tarehe 05/02/2020 na angalizo la Mvua kubwa kunyesha kwa baadhi ya maeneo ya mikoa ya Singida, Dodoma, Morogoro Kusini, Mbeya, Songwe, Njombe, Rukwa, Iringa na Ruvuma.
Kwa mujibu wa TMA, athari ambazo zinaweza kujitokeza ni pamoja na Baadhi ya makazi kuzungukwa na Maji, ucheleweshwaji wa usafiri, kusimama kwa muda baadhi ya shughuli za kiuchumi na kijamii.
Hivyo Mamlaka ya hali ya hewa nchini (TMA) imewataka wananchi kuzingatia taarifa na kujiandaa.
Utabiri wa Hali ya Hewa hatarishi wa siku Tano na Athari zinazoweza kutokea umetolewa leo tarehe 05/02/2020 na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.#UtabiriTZ pic.twitter.com/nPgweLHGJI
— Tanzania Meteorological Authority (@tma_services) February 5, 2020