Mke amsababishia kujiua
Mkazi wa Ubungo Maziwa aliyejulikana kwa jila la Festo Phiripo (40) mwanaume, juzi saa saba mchana alianguka ghafla toka chooni na kufariki papo hapo.
Amesema kulikuwa na ugonvi wa kifamilia kati ya marehemu na mke wake, baada ya marehemu kukopa kiasi cha shilingi za kitanzania 400,000 na kuzitumia kwa starehe.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Mwananyamala na upelelezi unaendelea.
Kamanda wa polisi kimkoa wa polisi Kinondoni Charles Kenyela, amesema chanzo cha kifo hicho inasadikiwa marehemu alikunywa sumu kwa mujibu wa maelezo ya mkewe Jesca Andrew (33).