Burudani
Mpoki atimuliwa Kili Awards Academy
Katika kile kilichokuwa kituko cha aina yake katika Kili Music Awards Academy iliyofanyika wikiendi hii iliyopita, mcheshi maarufu nchini Mpoki alijikuta akitimuliwa kutoka katika zoezi hilo.
Inasemekana kwamba, waratibu wa shughuli hiyo waligundua kwamba mcheshi huyo hakufaa kuwepo kati ya wapambanuaji wa nyimbo hizo kwa kuwa naye ni msanii wa muziki aliyerekodi wimbo hivyo kumfanya kutostahili kushiriki katika zoezi hilo.
Mpoki alikubaliana na maamuzi ya waandaji na kuondoka ukumbini hapo.