Michezo
Mshambuliaji wa Ghana, Andre Ayew asajiliwa Swansea City
Mshambuliaji wa kimataifa wa Ghana, Andre Ayew aliyekuwa akichezea klabu ya Marseille ya nchini Ufaransa amesajiliwa na klabu ya Swansea City ya England.
Mchezaji huyo sasa anasubiri kuidhinishwa kwa kibali cha ligi kuu ya England. Ayew, 25, ambaye alikuwa akivutia timu kadhaa za EPL na nyingine za Ulaya, amesaini mkataba wa miaka minne, baada ya mkataba wake kumalizika na klabu yake ya Ufaransa. Ayew atavaa jezi namba 10.