Michezo
Mtibwa Sugar yasajili kifaa kipya
Mshambuliaji wa Taifa , Kelvin Sabato ‘Kiduku’ amesaini klabu ya Mtibwa Sugar kwa mkataba wa miaka miwili.
Sabato ambaye msimu uliyopita alikuwa akiitumikia klabu ya majimaji jana jioni, ameingia kandarasi hiyo na Mtibwa ambayo inajiimarisha kwaajili ya msimu ujao.
Nyota huyo ni zao halisi la michuano ya Ndondo Cup akisajiliwa kwa mara ya kwanza kucheza ligi kuu akitokea kwenye moja ya timu iliyokuwa ikishiriki michuano hiyo.
By Hamza Fumo