Habari

Nchi zilizosaini mkataba wa nyuklia na Iran kukutana

Mataifa yaliyosaini mkataba wa nyuklia wa Iran yanakutana hii leo mjini Vienna, katika wakati ambapo Marekani ikishinikiza taifa hilo la Kiislamu lirejeshewe vikwazo na jumuiya ya kimataifa na kuongezewa vizuizi vya silaha.

Unraveling of Iran Nuclear Deal Exposes Europe's Weakness – Foreign Policy

Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, China na Urusi wanajaribu kuunusuru mkataba huo wa mwaka 2015 na Iran, ambayo imekuwa inaongeza shughuli zake za kinyuklia tangu mwaka jana.

Parties To Iran Nuclear Deal To Meet In Vienna Amid U.S. Pressure

Mkutano huo utaongozwa na afisa wa ngazi za juu wa umoja wa Ulaya Helga-Maria Schmid pamoja na manaibu waziri wa mambo ya kigeni ama wakurugenzi wa masuala ya siasa watakaohudhuria kutoka Uingereza, China, Ufaransa, Ujerumani, Iran na Urusi.

Umoja wa Mataifa wiki iliyopita ulizuia jaribio la Marekani la kurejesha vikwazo vya kimataifa dhidi ya Iran huku Washington ikishindwa kupata uungwaji mkono wa kuongeza vikwazo vya silaha kwa taifa hilo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents