Muziki
New Audio: Prince_Charz: Msanii anayetamba na RnB ya Kisukuma
Bongo Five inamtambulisha Msanii mkali wa muziki wa rnb anayeimba kwa Lugha ya Kisukuma, Charles Ndelah’Prince Charz’ kutoka Kanda ya Ziwa ameachiwa Wimbo wa Nakutogolwe (NAKUPENDA) ikiwa ni wimbo wake wa tatu baada ya ule wa Kisura wa Nzega na Sensema Malunde.
Charz Ndelaha amejipanga kufanya tour maalumu kwa ajili ya mikoa ya Kanda ya Ziwa kwa ajili ya kuzitambulisha nyimbo zake.
Nimejipanga kufanya mabadiko ya muziki kwa kuimba kwa lugha ya nyumbani, natamani sana kufanya kolabo na msanii Saida Karoli, Mrisho Mpoto, Wanne Star na wengineo.Kwa sasa ngoma zangu unaweza kuzipata kwenye Chaneli yangu ya You Tube kwa jina la Prince Charz au Charz Ndelah.