Michezo
Nilipokea ombi la kujiunga na klabu ya ligi ya Uingereza – Zlatan Ibrahimovic
Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya PSG nchini Ufaransa Zlatan Ibrahimovic amesema kuwa alipokea ombi la kujiunga na kilabu moja ya ligi ya Uingereza lakini akakataa kuthibitisha iwapo klabu hiyo ni Manchester United au la.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 ambaye kwasasa yuko huru baada ya kuondoka PSG na amehusishwa na uhamisho wa United.
Alipoulizwa iwapo ombi hilo linatoka Old Trafford ,alisema “Wacha tuone kitakachofanyika”
Kocha wa zamani wa Chelsea Jose Mourinho anatarajiwa kutangazwa kama kocha mpya wa Manchester United na alisha wahi kufanya kazi na Ibrahimovic alipkuwa katika kilabu ya Inter Milan