Habari

Obama kukamilisha ahadi ya kulifunga gereza la Guantanamo Bay

Marekani imetangaza kuwahamisha wafungwa 15 waliokuwa kwenye gereza la Guantanamo Bay nchini Cuba na kupelekwa Emirates.

Guantanamo Bay

Taarifa ya kuhamishwa kwa wafungwa hao imetolewa kutoka makao makuu ya jeshi la nchi hiyo lililopo Pentagon na kati ya wafungwa hao 12 wanatoka Yemen na watatu Afghanistan.

Kundi la watu hao ni moja kati ya kundi kubwa la wafungwa kuwahi kuhamishwa kutoka kwenye gereza hilo chini ya utawala wa Rais Barack Obama tangu mwaka 2008. Mpaka sasa idadi ya wafungwa waliobakia kwenye gereza hilo imefikia 61 hatua ambayo imeonekana kupingwa vikali na Chama cha Republican chini ya mgombea wake Donald Trump.

Hata hivyo mara kadhaa Rais Obama ameeleza masikitiko yake juu ya msimamo wa chama hicho wa kupinga mpango wake wa kutaka kufunga gereza hilo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake aliyowahi kuitoa wakati wa kampeni za Urais.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents