Burudani
Picha: Akon na Davido washiriki kwenye uzinduzi wa chuo kikuu cha kwanza cha muziki Afrika nchini Gabon
Pamoja na kuwa wenyeji wa kombe la mataifa ya Afrika, Gabon ni nyumbani kwa chuo kikuu cha kwanza cha muziki barani Afrika, (African Music Institute).
Uzinduzi rasmi wa chuo hicho kilichopo kwenye mji mkuu wa nchini hiyo, Libreville, ulimhusisha staa wa muziki Marekani mwenye asili ya Senegal, Akon, hitmaker wa Skelewu, Davido pamoja na maafisa wa chuo chuo Berklee, ambao ndio walioanzisha, African Music Institute.
Chuo hicho kitakuwa kikitoa shahada ya kwanza (degree), pamoja na shahada ya uzamili (masters) katika muziki.