Michezo
Picha: Ibada ya mwisho ya kuuaga mwili wa Ndikumana kabla ya mazishi
Wananchi wa Rwanda pamoja na wapenzi wa soka wa Afrika Mashiriki siku ya jana walipokea kwa mshituko mkubwa kifo cha ghafla cha aliyekuwa kapteni wa timu ya Taifa ya Rwanda, Hamad Ndikumana ambaye pia alikuwa ni mume wa muigizaji wa filamu nchini Tanzania, Irene Uwoya.
Umati mkubwa watu ulijitokeza katika msikiti wa Qaddafi huko Nyamirambo Rwanda kwaajili ya kumuaga mwanasoka huyo mkongwe. Angalia picha.
Ndikumana anadaiwa kufariki muda mchache baada ya kutoka mazoezi akiwa kama kocha wa timu ya Rayon Sports.
Bado ripoti ya madaktari haijatoka kueleza chanzo cha kifo chake.
Marehemu alikuwa na mtoto mmoja aliyezaa na aliyekuwa mke wake muigizaji wa Tanzania, Irene Uwoyo.
Source: Newtimes