Picha: Joh Makini afanya collabo na rapper number 3 au 2 kwa ubora Afrika Kusini
Ukiambiwa utaje rappers watatu bora kwa sasa nchini Afrika Kusini, huwezi kuacha kuwataja AKA, Cassper Nyovest na K.O.
K.O
Katika kuonesha kuwa Weusi hawataki kabisa mchezo mwaka huu, Joh Makini ameingia studio kurekodi wimbo na rapper wa kundi maarufu la Afrika Kusini la Teargas, Ntokozo Mdluli maarufu kama K.O.
Joh Makini na K.O wakiwa studio
Joh Makini ambaye yupo jijini Johannesburg alikoenda pamoja na G-Nako, Vanessa Mdee na Navy Kenzo, amepost picha Instagram akiwa na K.O na kuandika: #Studio_flow with #KO @mrcashtime himself #2KINGS #ARUSHA_MEETS_JOHANNESBURG #2015 #GODENGINEERING #WEUSIMEETSCASHTIME #amonmyway.”
Joh Makini akiwa na mtangazaji wa MTV Base, Nomuzi Mabena
Hivi karibuni K.O alihit na ngoma ‘Caracara’ aliyomshirikisha Kid X.
Pia ameshirikishwa na AKA kwenye hit single yake ‘Run Jozi’