Michezo
Picha: Klabu ya Simba SC ya zindua duka la kuuza vifaa vya michezo
Klabu ya Simba SC ya Jijini Dar es Salaam, wamezindua rasmi duka ambalo litakuwa linauza vitu mbalimabali vyenye nembo ya klabu hiyo kwa lengo la kutengeneza pesa.
Rais wa klabu ya Simba (katikati) akikata utepe kuzindua duka la kuuza vifaa vya Simba ambalo lipo Dar Free Market Mall Ground Floor
Rais wa Simba Bw. Evans Aveva amezindua rasmi duka la Simba ambalo lipo katika jengo la Dar FRee Market, eneo la Oysterbay, litakuwa likiuza vifaa vya michezo, jezi, kofia, T-shirts pamoja na vitu vingine vingi vyenye chapa ya Simba kwa ajili ya kujiingia kipato kutokana na chapa ya timu yao.