Michezo
Picha: Muonekano wa Uwanja mpya wa Santiago Bernabeu ifikapo 2020
Picha za uwanja wa Santiago Bernabeu kuja na muonekano mpya ifikapo mwaka 2020 klabu ya Real Madrid, imeamua kufanya Marekebisho ya uwanja wao ambao utagharimu Pauni Milioni 360 hadi kukamilika, marekebisho hayo yataufanya uwanja huo kuwa katika mwonekano wa kibiashara.
Rais wa Real Madrid Florentino Perez alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu marekebisho ya Uwanja huo
Uwanja huo pamoja nakufanyiwa marekebisho hayo, bado utaendelea kuwa na uwezo wa kuingiza watu 80,000 na ofisi za klabu hiyo ambazo zipo katika uwanja huo zitahamishwa ili kupisha upanuzi wa sehemu ya makumbusho ya klabu.