Burudani
Picha: Si Will Smith tu aliyekuja Serengeti, ni pamoja na supermodel Chanel Iman
Tanzania ina ugeni mzito wiki hii.
Muigizaji mashuhuri wa filamu, Will Smith amekuja nchini kwaajili ya mapumziko. Staa huyo wa Suicide Squad, yupo kwenye mbuga ya wanyama ya Serengeti akifurahi uumbaji wa Mungu.
Hata hivyo imebainika kuwa Smith si staa pekee wa Marekani aliyepo Tanzania. Supermodel wa Marekani, Chanel Iman naye amejumuika.
Mrembo huyo amekuja na boyfriend wake.
Kwenye Instagram, amepost picha akiwa na Will Smith mbugani Serengeti na kuandika: Great places with great friends and Will is One of the coolest.”
Kuna uwezekano kuwa wote wamekuja kwenye msafara mmoja.