Picha: Simba walivyoibuka washindi wa Mtani Jembe 2013 kwa kuifunga Yanga goli 3 -1
Wekundu wa Msimbazi, Simba Sport Club jana waliibuka washindi wa mechi ya Mtani Jembe 2013 kwa kuwafunga watani wao wa jadi Yanga African goli 3-1 katika mechi iliyochezwa katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Wekundu wa Msimbazi Simba Sport Club wakishangilia pamoja na kombe lao
Mchezo huo maalum wa kufunga promotion ya ‘Nani Mtani Jembe 2013’ lililoandaliwa na Kilimanjaro Premium Lager umewafanya Simba kuibuka na kombe hilo,medali pamoja na hundi ya shilingi milioni 1,061,600 iliyotokana na mashabiki wa Simba kunywa bia ya Kilimanjaro na kutuma ujumbe wa namba kwa timu yao.
Yanga baada kufungwa goli 3-1 na Simba katika mechi hiyo ameibuka na kombe dogo,medali pamoja na shilingi milioni 98,938,400 zilizotokana na mashabiki wa Yanga kunywa bia ya Kilimanjaro na kutuma ujumbe wa timu yao.
Magoli ya simba yaliwekwa kimiani na mshambuliaji wake mahiri mwenye kasi nyingi na mbinu lukuki za ufungaji Hamisi Tambwe aliYEpachika magoli 2 huku bao la tatu likifungwa na mchezaji aliyesajiliwa dirisha dogo kutoka Mtibwa Awazi Juma. Goli la Yanga lilifungwa na Emmanuel Okwi kwa kichwa.
Wachezaji wa Simba wakishangilia
Kocha mkuu wa Yanga na wasaidizi wake kabla ya mechi kuanza.
Kocha wa makipa wa Yanga akiwapa mazoezi makipa wa Yanga
Kocha wa Simba Zdravko Logarusic akiwa na wasaidizi katika benchi la ufundi la Simba
Kocha wa Simba Zdravko Logarusic akifikiria jambo kabla ya mechi kuanza
Kikosi cha Simba kilichoipoteza Yanga kwa magoli 3-1
Meneja wa Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe ambao ni wadhamini wa promotion ya Nani Mtani Jembe akikabidhi hundi ya pesa kwa viongozi wa Yanga
Okwi akisalimia mashabiki wa Yanga baada ya kuingia uwanjani
Shabiki akikimbizwa hospitali baada ya kuzimia
Mgeni rasmi Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe akikabidhi kwa Simba kombe la ushindi
Simba walianza mchezo kwa dua maalum
Waigizaji wa filamu ambao ni mashabiki wa Yanga Shamsa Ford na Maya wakifuatila mpira kwa makini
Wekundu wa Msimbazi wakishangilia na kombe lao
Simba wakikabidhiwa hundi yao ya shilingi milioni 1,061,600 zilizotokana na promotion ya Nani Mtani Jembe
Yanga wakikabidhiwa hundi yao ya shilingi milioni 98,938,400