Burudani

Picha: Staa wa tamthilia ya Empire atua Bongo kusaidia wakimbizi

Staa wa filamu kutoka Marekani Nitara Carlynn Long maarufu kwa jina la Nia Long amewasili nchini wiki hii.

Nia amewasili na muigizaji mwenzake anayefahamika kama Massai Dorsey. Wawili hao wameletwa na shirika linalowashughulikia wakimbizi duniani UNHCR kwa ajili ya kutoa elimu ya madhara ya ugonjwa wa Malaria katika kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyopo mkoani Geita.

Muigizaji huyo ambaye pia ameonekana katika episode nane za tamthilia ya Empire, kupitia mtandao wa Instagram ameonyesha kufurahia ziara hiyo kwa kuandika, “Meet my new little friend! Today we distributed nets to her family and I learned how to make cassava.”

“I hope you’ll join me in this journey with @nothingbutnetsofficial and the @UNHCRTanzania @refugees team: Nothingbutnets.net/nia,” ameongeza.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents