Michezo
Picha: Lewis Hamilton aonesha gari lake la kifahari kusherehekea ushindi wa Monza Italia Grand Prix
Bingwa wa mbio za magari za Formula One, Lewis Hamilton alishinda ubingwa wake wa saba Jumapili kwenye mashindano ya Monza Italia Grand Prix.
Baada ya ushindi huo, Hamilton ameonekana kujipongeza akiwa na gari lake jipya la kifahari, kitu kinachotafsiriwa kama sehemu ya kusherehekea ubingwa wake huo.
Hamilton ameonekana katika picha akiwa na gari la kifahari la Mercedes G63 AMG ambalo thamani yake inatajwa kufikia pound 370,000 ambazo ni zaidi ya shilingi bilioni 1 za Kitanzania.