Burudani
Poleee: Madonna ala mweleka mbaya wakati akitumbuza kwenye Brit Awards (Picha)
Madonna alirejea jana kwenye Brit Awards kwa mara ya kwanza tangia miaka 20 iliyopita lakini mambo yalitaka kumharibikia.
Mwanzoni mwa performance yake, Madonna alianguka kwenye ngazi jukwaani hapo baada ya kofia ndefu aliyokua ameivaa kuvutwa na dancer wake. Kofia hiyo ilipaswa kuondolewa kirahisi lakini dancer huyo alimvuta pia Madonna.
Kitendo hicho kilimfanya hadi aiangushe microphone na kushindwa kuimba baadhi ya mashairi. Baada ya kuinuka na kuchukua mic sauti yake ilisikika ikiwa tofauti kidogo. Baadaye Madonna alitumia Instagram kuandika: Thanks for your good wishes! I’m fine!.”
Picha zaidi hapo chini.