Habari
Rais wa Bolivia na makamu wake watangaza kujiuzulu, wananchi waingia barabarani na kusherehekea maamuzi yao (+video)
Rais wa Bolivia Evo Morales ametangaza kujiuzulu kupitia hatuba yake na luninga. Uamuzi huo unakuja muda mchache baada ya uchunguzi uliyofanywa na OAS juu ya matokeo ya uchaguzi wake ambao ulitangaza kuwamshindi mwezi uliyopita kugubikwa na udanganyifu.
Evo Morales ametangaza hatua hiyo siku ya Jumapili kwamba amewasilisha barua yake ya kujiuzulu bungeni baada ya jeshi, polisi na upinzani kumtaka kufanya hivyo.
“Matamanio yetu makubwa ni kuona amani inarejea kwa watu wetu,” amesema Morales katika luninga wakati huo huo makamu wake wa rais Alvaro Garcia Linera naye akitangaza kujiuzulu kwake.
“Ninaomba kuacha kushambuliana, kuacha kuchoma vitu na kushambuliana,” Morales alipowaambia watu wa Bolivian.