Michezo

Real Madrid wageuka vibonde barani Ulaya, watupwa nje ya michuano ya UEFA nyumbani kwao

Klabu ya Real Madrid imetupwa nje ya michuano ya klabu bingwa barani Ulaya kwa kukubali kichapo cha goli 4-1 dhidi ya Ajax FC.

Hii inakuwa mara ya kwanza kwa Ajax kufuzu robo fainali ya michuano hiyo tangu msimu wa mwaka 2002/03.

Matokeo mengine ya usiku wa UEFA ni Spurs wameiadhibu Borusia Dortmund kwa goli 1-0 na kufanikiwa kutinga hatua ya robo fainali.

Kwenye mchezo wa kwanza Spurs waliwachakaza Dortmund goli 3-0 .

Huu unakuwa mchezo wa nne kwa Real Madrid kufungwa nyumbani kwao mfululizo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents