Michezo
Rooney kucheza kwa masharti United
Aliyekuwa mchezaji wa timu ya taifa ya Wales na klabu ya Manchester United, Ryan Joseph Giggs amesema, Wayne Rooney ataweza kusalia katika kikosi cha United endapo atakubaliana na masharti ya kutochezeshwa kila mchezo utakao ikabili timu hiyo.
Mchezaji wa timu ya taifa ya Uingereza na klabu ya Man Unite, Wayne Rooney akionekana kuchukizwa na kutopangwa katika timu yake
Rooney ambaye hakukata tamaa katika msimu wa mwaka 2016/17 baada ya kutochezeshwa katika michezo kadhaa chini ya kocha, Jose Mourinho alikaririwa akisema kuwa angeamua hatima yake baada ya kumalizika kwa ligi kuu nchini Uingereza lakini mpaka sasa mchezaji huyo ameshindwa kuonyesha dalili yoyote ya kuondoka United.
BY HAMZA FUMO