Jana tamasha la Miss Dar Inter College limefikia mwisho baada ya kuibuka mshindi, Rose Msuya kutoka chuo cha Usimamizi wa Fedha ‘IFM’ na kufuatiwa na Blessing Ngowi na kuwa na nafasi nzuri ya kuingia kwenye kinyanyiro kingine cha kuwania Miss Tanzania.
Rose Msuya akivishwa taji la mwaka 2011 kwenda 2012na mshindi aliyepita
Majaji wakiangalia pambano la warembo.
Warembo walioingia katika kinyanyiro cha tano bora alikuwa ni Blessing Ngowi (16) mshindi wa pili , Glory Peter (13) mshindi wa tatu, Rose Msuya (14) mshindi wa kwanza, Winfrida Raymond (1) mshindi wa tano na Eliza Aloyce (11) mshindi wa nne
Warembo wakicheza wimbo wa Bongo Fleva kutoka kwa Dully Sykes
Katika tamasha hilo, mwanamuziki wa kizazi kipya Dully Sykes, alikuwa akiburudisha mashabiki wake.