Burudani

Show ya Wizkid jijini Kampala Jumamosi hii yaahirishwa, waandaji watoa sababu hii

Mashabiki wa muziki jijini Kampala, Uganda, wamesikitishwa na taarifa kuwa show ya Wizkid iliyokuwa imepangwa kufanyika Jumamosi hii haitokuwepo tena licha ya maandalizi makubwa yaliyokuwa yamefanyika tayari.

14504684_207159059741402_4967743853852360704_n

Waandaji wa show iliyokuwa imepewa jina ‘6 Years of Startimes; Wizkid Live in Kampala’, wamedai kuwa staa huyo wa Nigeria alishindwa kusafiri na ndege kutoka Marekani usiku wa Alhamis hii kutokana na sababu ambazo zilikuwa juu ya uwezo wake.

15043399_639920036186278_1155985474146271232_n

Waandaji hao ambao ni Face TV, wamewaomba radhi mashabiki na wadhamini wa show hiyo kufuatia hatua hiyo. Show hiyo ilikuwa imepangwa kufanyika kwenye uwanja wa Lugogo Cricket.

cymn4gnwgaapm3k

Wamedai kuwa wanaendelea kuwasiliana na Wizkid ili kupanga tarehe mpya ya show hiyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents