Mshindi wa tatu wa Miss Tanzania 2014, Jihan Dimachk, amesema hajawahi kujutia kushiriki shindano hilo.
Jihan alishiriki kwenye shindano hilo ambalo liligubikwa na skendo nzito baada ya Sitti Mtemvu kushinda. Skendo hiyo ya kudanganya umri, ilipelekea kufungiwa kwa shindano hilo kwa miaka miwili. Limerejea tena mwaka huu.
Jihan amedai kuwa Miss Tanzania imempa exposure kwa kazi zake za uanamitindo. Pamoja na kuendelea na shughuli hizo, pia mrembo huyo ni mfanyakazi.