Simba SC yaonesha matumaini kwa Watanzania Kombe la Shirikisho Afrika
Klabu ya Simba huenda ikawatoa kimasomaso Watanzania kwenye michuano mikubwa barani Afrika ya Kombe la Shirikisho kutokana na ushindi mnono wa leo wa goli 4-0 dhidi ya klabu ya Gendamarie Tnale kutoka nchini Djibouti.
Magoli ya Simba yamefungwa na John Bocco 33′, 44′ , Emannuel Okwi 90+ na Said Ndemla kunako dakika ya 2 ya mchezo.
Kwa ushindi huo hakuna shaka kuwa Simba watafanikiwa kusonga mbele kwenye mchezo wa marudiano hii ni kwa jinsi kikosi cha Gendamarie Tnale kilivyo hakitakuwa na uwezo wa kumtwanga mnyama goli 5-0 ili kusonga mbele ingawaje mpira haupo hivyo ila Simba wameonesha matumaini kwa Watanzania.
Hayo yamejiri wakati ambapo mahasimu wao Klabu ya Yanga jana wamepata ushindi mwembamba wa goli 1-0 dhidi ya St Louis mchezo wa klabu bingwa Afrika raundi ya kwanza uliopigwa uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.