Habari
Spika wa Tanzania kuwa Mwanamke
Kamati kuu ya Chama Cha Mapinduzi, kimewateua wanawake, watatu kati ya wabunge 13 waliokuwa wakiwania nafasi ya spika wa bunge wa Jamhuri ya Tanzania.
Hayo yalisemwa na katibu mkuu wa Chama hicho, Bw. Yusuf Makamba akitaja majina yao kuwa ni; Mh. Anna Abdallah, Mh. Kate Kamba na Mh. Anna Makinda.
Makamba alisema kwamba CCM imeamua kwa makusudi kabisa kumteua mwanamke kuongoza moja kati ya mihimili ya taifa la Tanzania na kuweka historia kuwa ni mwanamke wa kwanza kushikilia nyadhifa hiyo.