Stereo amshirikisha Victoria Kimani, wimbo unaitwa ‘Wako’ (I Will Never Let U Down)
Rapper Stereo aliye chini ya kampuni ya Unity Entertainment ya AY amefanya collabo yake ya kwanza ya kimataifa na msanii Victoria Kimani wa Kenya.
Stereo amesema collabo ya wimbo ‘Wako’ akiwa na Victoria inaweza kumuweka vizuri kimuziki katika ukanda wa Afrika Mashariki.
“Nimefanya collabo yangu ya kwanza ya kimataifa na Victoria Kimani nikiwa chini ya Unity Entertainment,AY ndio aliyoweza kuunganisha mpaka nikafanya hii collabo,@ Stereo ameiambia Bongo5. “Kwahiyo wimbo unaitwa Wako (I Will Never Let You Down) na umefanyika katika studio za Bongo Records na P.Funk Majani. Wadau wakae mkao wa kula.Collabo yangu na Victoria naona nimefanya au Unity Entertainment imefanya uamuzi mzuri ukiangalia Victoria ni msanii mkubwa Afrika, kwahiyo naona itaniweka zaidi kibiashara katika muziki wa Afrika Mashariki.”