TFF kumchukulia hatua mchezaji ‘anayewapiga dole’ wenzie uwanjani, Juma Nyoso
Cheza mbali na Juma Nyoso lasivyo atakupiga dole!
Camera zilimnasa Nyoso akimpiga dole mchezaji wa Azam, Bocco
Beki huyo wa Mbeya City amerudia tena kitendo hicho cha kudhalilisha wachezaji wenzake wake uwanjani kiasi ambacho TFF imeahidi kumchukulia hatua kali zaidi awamu hii.
“Udhalilishaji uliofanywa leo na mchezaji mmoja wa timu ya ligi kuu tumeuona,hatua kali zitachukuliwa muda sio mrefu,tuwe na subira,” Rais wa TFF, Jamal Malinzi ameandika kwenye Twitter.
Udhalilishaji uliofanywa leo na mchezaji mmoja wa timu ya ligi kuu tumeuona,hatua kali zitachukuliwa muda sio mrefu,tuwe na subira.
— Jamal Malinzi (@jamalmalinzi) September 27, 2015
Awamu hii Nyoso amempiga ‘dochi’ mchezaji wa Azam, John Bocco kwenye mchezo wa Azam na Mbeya City jana.
Nyoso amewahi pia kumfanyia kitendo hicho mshambuliaji wa Simba, Elius Maguri na TFF kumwadhibu.