TID na Top Band ndani ya Bilicanas
Top Band ya TID ikitoa burudani ya kila Jumanne pale Club Billcanas, hapa akionyesha uwezo wake wa kuimba na kusakata rhumba.
TID alisema hana mpango wa kuongeza waimbaji wala wapiga chombo chochote kwenye band yake, kwakuwa wanamuziki wote hao anawapata kwa njia ya kuwakodi kwaajiri ya show iliyopo.
Baadhi ya waimbaji na wapigaji vifaa mbali mbali vya muziki, wakiwa katika hari ya kuimba na kutoa buludani kwa mashabiki wao, hebu angalia jinsi walivyokuwa katika pozi la kibuludani pale Billcanas.
Bushoke naye alikuwepo katika show hiyo hapo Billcanas, akipata burudani toka Top Band, hata hivyo alisema na yeye yupo ‘bize’ kwaajili ya kukamilisha bendi yake.
Anasema bendi hiyo itakuwa moto wa kuotea mbali, na baadhi ya nyimbo zake ambazo alishaziimba zamani kama Solo artist sasa hivi atazifanya kama bendi ili kuleta ladha tofauti kwa mashabiki wake.
Ikafika zamu ya Kushow love na Bongo5, na ndipo nikakutana na ‘Hassan Moshi au Tx Jr’.
Naye akatudokezea machache, kwamba amesharudi kwenye bendi ya nyumbani kwa hivyo mashabiki wake wakae mkao wa kula. Wasubiri vitu vipya ambavyo bado vipo jikoni, akiwa katika bendi ya nyumbani Msondo Ngoma band baada ya kutoka FM Academia.
Tukashow Love na mashabiki wa Bongo5, cio……..