Jana Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania walijumuika kutimiza haki zao za kupiga kura kwa viongozi kuanzia ngazi ya Udiwani, Ubunge na nafasi ya Rais.
Ingawa kuna matatizo yalibainika kutoka kwa Tume ya uchaguzi taifa, kama vile kukosekana kwa majina ya baadhi ya wapiga kura na pia kuchelewa kuwepo wasimamizi kwenye zoezi la upigaji kura, siku ya jana ilienda kwa amani kama ilivyokusudia.
Habari za kuaminika zinasema kwamba, mpaka sasa Chama tawala CCM, Chama cha Mapinduzi na Upinzani Chadema zinakabana koo kwa kile kinachosadikika kuwa kukaribiana sana kwa kura kati yao.
B5 iko kwenye harakati za kupata matokeo ya uhakika ili tuweze kuyapost mtandaoni.
Mungu Ibariki Tanzania.