Burudani

Ufafanuzi wa Vanessa Mdee kuhusu ngoma zake na Diamond kuchezwa Nigeria

Msanii wa muziki Bongo, Vanessa Mdee ametolea ufafanuzi kauli yake iliyodai alipofika Nigeria alikuta ngoma za wasanii toka Bongo zinazochezwa ni zake na za Diamond.

Baada ya kauli hiyo Vanessa amekuwa akishambuliwa na mashabiki hasa wa team Kiba kuwa kauli yake ni yenye upendeleo kwa upande mmoja. Kupitia Instagram Vanessa ameamua kumjibu shabiki aliyehoji kuhusu hilo.

vanessamdee @ze_masta my love hiyo issue nilikuwa nazungumza kitu kikubwa zaidi lakini wenye akili zao wamegeuza imekuwa hivyo. Na Ukiangalia lengo la jibu langu ilikuwa kuwahamasisha waTanzania wathamini na waPromote zaidi mziki wa home maana wenzetu ndivyo wanavyofanya.

Sasa wapi hapo nimemdiss kaka? Kaka anajua mimi shabiki yake sasa tutafika kweli kila neno linageuzwa kuwa negative when in truth I was just shedding light on what I was seeing. Jamani.

Hapo Jux Vanessa aliiambia Clouds Fm alipoenda Nigeria kwa ajili ya kutangaza albamu yake ‘Money Mondays’ katika moja club alizopita alikuta ngoma zinazochezwa kutoka Bongo ni ya Patoranking na Diamond ‘Love You Die’ na ile aliyoshirikiana na Reekado ‘Move’.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents