Burudani

Utafiti: Asilimia 95 ya Watanzania wanataka kuwepo haki ya kuikosoa serikali

Asilimia 95 ya wananchi wa Tanzania wamedai kuwepo na haki ya wananchi kuikosoa serikali.

twaweza-colour-logo

Wananchi hao ni pamoja na wafuasi wa chama tawala na wale wa upinzani, kwa mujibu wa utafiti mpya wa taasisi ya Twaweza. Matokeo ya utafiti huo uliopewa jina Sauti za Wananchi: Demokrasia, Udikteta & Maandamano, umezinduliwa Alhamis hii jijini Dar es Salaam.

ctgmg1owaaahxhb

Umebaini kuwa 93% ya wafuasi wa chama tawala wangependa wananchi waruhusiwe kuikosoa serikali inapofanya makosa.

Utafiti huo pia umeonesha kuwa 11% ya wananchi wanaamini kwamba Tanzania inaongozwa na dikteta, huku 58% wakipinga. Pia umedai 29% ya wananchi walio karibu na vyama vya upinzani wanaamini Tanzania inaongozwa na dikteta.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents