Uzinduzi wa dawa mpya ya Malaria
MWANAMUZIKI bora aliyetwaa tuzo mbili Zanzibar katika Zenji Fleva, alichukua tuzo za mwanamuziki bora wa mwaka na wimbo bora wa mwaka kwa upande wa Zanzibar Sultan King, akiwa wapa mkono mgeni rasmi katibu mkuu wa wizara ya Afya M . Salehe Udawi na baadhi ya viongozi walioudhuria katika tamsha la ufunguzi wa dawa za MALARI kwa bei nafuu katika maduka na Hospitali Binafsi kwa Zanzibar tu katika viwanja vya kufanyia mikutano Matumbaku.
Katika uzinduzi wasanii mbalimbali, walikuwepo kwaajili ya kuunga mkono .
Hapa mwanamuziki Sultani King akiimba kwa hisia.
Baby J naye alikuwepo kwaajili ya kutoa Show ya nguvu na madensa wake, naye aliweza kuwashika vizuri tu.
Hlima na Dodo wakiimba mashairi yaliyokuwa yakiamasisha watu kwendfa kupima na kutumia dozi kwa ukamilifu, pia kuwatoa hofu na mashaka juu ya dawa hizo.
Kikundi cha sanaa cha Maisha Huru Group cha Zanzibar nacho kilitoa igizo fupi, lenye kutoa elimu juu ya utumizi sahihi wa dawa za MALARIA, na mama mjamzito kuwahi Hospitali pindi tu anapohisi homa.
Sultan Kingi akiimba juu ya jukwaa
Wasanii mbalimbali wa Zenji Fleva, wakati bara wanaita Bongo Fleva na hapa wakisubiri kupanda jukwaani akiwemo na Sultani King