BurudaniDiamond Platnumz
Video: Diamond, Mohombi, Davido na Lumino washoot video ya remix ya Rockonolo Gabon, itafanyika Bongo pia
Rockonolo, wimbo ambao Diamond, Mohombi na Lumino waliutumbuiza Jumamosi kwenye ufunguzi wa kombe la mataifa ya Afrika, AFCON 2017, nchini Gabon, unaweza kuwa moja ya nyimbo kubwa za Afrika mwaka huu.
Wimbo huo ni wa Lumino na amewashirikisha mastaa hao kwenye remix yake.
Jumapili hii, mastaa hao wameshoot video yake na kumwalika staa wa Nigeria, Davido kuungana nao.
Haijaishia hapo tu, Diamond amedai kuwa Jumanne hii pia watashoot vipande vingine vya video hii jijini Dar.
“Leo tulifanikiwa kushoot video ya #Rockonolo Remix GABON… tutashoot pia vipande kadhaa nchini Tanzania siku ya Jumanne, je ungependa kuwa mmoja wapo?” ameandika kwenye Instagram.
Hajaeleza iwapo Mohombi na Lumino nao watakuja Dar kwaajili ya kushoot vipande hivyo.