Habari
Viongozi wa dunia kukutana kwenye mkutano UN Jumanne hii
Viongozi wa dunia Jumanne hii wanakutana kwenye mkutano wa mwaka wa Umoja wa Mataifa kujadili masuala muhimu yanayohitaji suluhu.
Miongoni mwa masuala muhimu yatakayojadiliwa ni pamoja na mgogoro wa Syria, kuongezeka kwa mashambulio duniani ya kundi la ISIS, vita na umaskini. Mkutano huo utakutanisha viongozi wakuu wa nchi 135 pamoja na mawaziri 50. Utamalizika Sept. 26.
Katika Mkuu wa umoja huo, Ban Ki-moon anayemaliza muda wake Dec. 31, na Rais wa Marekani, Barack Obama anayemalizia muda wake mwaka huu, watahutubia umoja huo wenye wanachama 193 kwa mara ya mwisho.